Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo TFF yafungua dirisha la usajili
Michezo

TFF yafungua dirisha la usajili

Alfred Lucas, msemaji wa TFF
Spread the love

SHIRIKISHO la soka nchini Tanzania (TFF), limetangaza kufungua rasmi dirisha la usajili wa wachezaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara, 2017/2018 kuanzia leo 15 Juni mpaka tarehe 6 Agosti, 2017, anaandika Shafiyu Kyagulani.

Alfred Lucas, msemaji wa TFF amewambia wanahabari kuwa kufunguliwa kwa dirisha la usajili kutatoa fursa kwa klabu za ligi kuu kufanya usajili ingawa tayari baadhi ya klabu zilishaanza kusajili kabla ya ufunguzi wa dirisha hilo.

Tayari klabu ya Yanga imeripotiwa kumnasa Abdallah Ally Shaib (Ninja) kutoka Jang’ombe FC ya Zanzibar huku Kagera Sugar ikimsajili beki wa kati Juma Nyoso na Simba SC wakiripotiwa kuwanasa John Bocco, Shomari Kapombe na mlinda mlango Aishi Manula – wote kutoka Azam FC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!