Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko TCU watia kitanzi vyuo viwili
Habari Mchanganyiko

TCU watia kitanzi vyuo viwili

TCU
Spread the love

TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imevifuta vyuo vikuu viwili kikiwemo cha Mtakatifu Yohana (SJUT) kilichopo Msalato Dodoma na Theophil Kisanji (TEKU) cha Tabora na kusitisha utoaji mafunzo katika vyuo vikuu vitano. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 25 Septemba 2018 jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amevitaka vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo kuwahamisha wanafunzi katika vyuo vilivyositishwa kuhamishwa katika vyuo vingine kabla ya muhula wa mwaka wa masomo wa 2018/19 kuanza.

Profesa Kihampa, amevitaja vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo ikiwemo Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB), Chuo Kikuu cha Eckernford Tanga (ETU), Chuo Kikuu cha Mlima Meru, Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta kituo cha Arusha (JKUAT-Arusha Center) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah Kibira (JOKUCo).

Amesema vyuo hivyo viko katika uangalizi maalum na kwamba haviruhusiwi kudahili wanafunzi wapya kwa ngazi zote za masomo kuanzia Astashahada, Stashahada, Shahada, Shahada ya uzamili na uzamivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!