Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCU watia kitanzi vyuo viwili
Habari Mchanganyiko

TCU watia kitanzi vyuo viwili

TCU
Spread the love

TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imevifuta vyuo vikuu viwili kikiwemo cha Mtakatifu Yohana (SJUT) kilichopo Msalato Dodoma na Theophil Kisanji (TEKU) cha Tabora na kusitisha utoaji mafunzo katika vyuo vikuu vitano. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 25 Septemba 2018 jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amevitaka vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo kuwahamisha wanafunzi katika vyuo vilivyositishwa kuhamishwa katika vyuo vingine kabla ya muhula wa mwaka wa masomo wa 2018/19 kuanza.

Profesa Kihampa, amevitaja vyuo vilivyositishwa kutoa mafunzo ikiwemo Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB), Chuo Kikuu cha Eckernford Tanga (ETU), Chuo Kikuu cha Mlima Meru, Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta kituo cha Arusha (JKUAT-Arusha Center) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah Kibira (JOKUCo).

Amesema vyuo hivyo viko katika uangalizi maalum na kwamba haviruhusiwi kudahili wanafunzi wapya kwa ngazi zote za masomo kuanzia Astashahada, Stashahada, Shahada, Shahada ya uzamili na uzamivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!