Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yaripoti kifo cha kwanza mgonjwa wa Corona
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanzania yaripoti kifo cha kwanza mgonjwa wa Corona

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeripoti kifo cha kwanza cha Mgonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Taarifa ya kifo hicho imetolewa leo tarehe 31 Machi 2020 na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Taarifa ya Waziri Ummy inaeleza kuwa, kifo hicho kimetokea alfajiri ya leo katika Kituo cha Matibabu ya Wagonjwa wa COVID-19, kilichopo Mloganzila jijini Dar es Salaam.

Waziri Ummy amesema marehemu alikuwa mwanaume mwenye umri wa miaka 49, ambaye alikuwa anasumbuliwa na maradhi mengine.

“Ninasikitika kutangaza kifo cha kwanza cha mgonjwa wa COVID-19 hapa nchini kilichotokea alfajiri ya leo katika kituo cha matibabu ya wagonjwa wa COVID-19 kilichopo Mloganzila. Marehemu ni Mtanzania  ambaye pia alikuwa anasumbuliwa na maradhi mengine,” inaeleza taarifa ya Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema hadi kufikia leo idadi ya wagonjwa wa COVID-19 nchini ni 19, ambapo aliyepona ni mmoja na aliyefariki dunia mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!