SERIKALI imeiomba Benki ya Dunia (W.B) msaada wa fedha kiasi cha dola 100 milioni kwa ajili ya kukamilisha mradi wa ujenzi wa bonde la mto Msimbazi jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ombi hilo leo tarehe 25 Februari 2019 jijini Dar es Salaam na Suleiman Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI wakati akizungumza na maofisa wa W.B.
Jafo ameeleza kuwa, ni muhimu bonde hilo kufanyiwa marekebisho kutokana kwamba limekuwa chanzo cha vifo vya baadhi ya watu na uharibifu wa mali kwa sababu ya mafuriko yanayotokea wakati wa msimu wa mvua.
“Dola milioni 100 zinahitajika kukamilisha mradi wa kuboresha bonde hilo, ni matumaini yangu Benki ya Dunia mtashirikiana nasi kama am,bavyo tunashirikiana katika miradi mingine ya maendeleo,” amesema Jafo.
Maofisa wa ngazi mbalimbali wa Benki ya Dunia wako nchini kwa muda wa siku mbili kuanzia leo hadi kesho tarehe 26 Februari 2019 kwa ajili ya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayoendelea ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Leave a comment