Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tanzania yaanza kupata kibano cha kimataifa
Habari za SiasaTangulizi

Tanzania yaanza kupata kibano cha kimataifa

Spread the love

KIBINYO kinachotokana na hatua ya serikali kugandamiza demokrasia nchini, kimeanza kuutafuna utawala wa sasa. Anaripoti Mwandishi Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa kutoka mataifa kadhaa ya Marekani na Ulaya zinasema, karibu mataifa yote ya maeneo hayo, ikiwamo Sweden, yanaitilia shaka amani ya Tanzania na kupoteza sifa ya kuwa baba wa demokrasia Afrika, tofauti na ilivyokuwa miaka sita iliyopita.

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Finland na Denmark, Dk. Willibroad Slaa amesema, hatua ya baadhi ya watu kuituhumu serikali ya Rais Magufuli, kukandamiza uhuru wa kujieleza na uhuru wa kutoa maoni, “kunawapa shida mabalozi kuitetea nchi huko walipo.”

“Vitendo hivyo vinawakatisha tamaa wahisani wanaotaka kuisaidia Tanzania. Wahisani wanaogopa kuleta fedha nchini na kwa kweli, hali yetu kisiasa kwenye mataifa ya nje, siyo nzuri,” ameeleza.  

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja katika kipindi ambacho taasisi kadhaa za ndani ya nchi, vikiwamo vyama vya siasa na mashirika ya madhehebu ya kidini, wakiituhumu serikali “kukandamiza uhuru wa wananchi wa kujieleza na kutoa maoni.”

Katika maelezo yake ambayo aliyatoa kwenye mahojiano yake na kituo cha televisheni cha Star TV, Dk. Slaa amesema,  watalii zaidi ya 100 kutoka Sweden wameahirisha safari ya kuja nchini  kwa ajili ya kutalii.

Alimtuhumu kiongozi mmoja, ambaye hakumtaja jina kwa kusema, “…kauli za kiongozi mmoja, zimesababiha madhara makubwa kwa nchi.” 

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo katika mahojiano yake na kituo cha televisheni cha Star tv. Dk. Slaa ambaye aliwahi kuwa katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendelo (Chadema), alitoa kauli hiyo, wakati wa ziara ya mabalozi wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali duniani walipotembelea mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR eneo la Soga, mkoani Pwani.

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi kadhaa duniani, wapo katika ziara ya kutembelea na kuijonea utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa fedha za ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!