KAMISHNA wa Magereza Tanzania, Jenerali Suleiman Mzee ameikabishi klabu ya Tanzania Prisons basi dogo aina ya Toyota Coaster itakayotumika na timu hiyo katika michezo mbalimbali ikiwamo Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Katika makabidhiano hayo Mkuu wa sehemu ya michezo ndani ya jeshi hilo SSP Matrida Mlawa amesema kuwa wanamshukuru Jenerali Mzee kwa kuwapatia usafiri huo ambao utaisaidia timu na kutatua changamoto za usafiri.
“Tunamshukuru Jenerali wa Magereza, Kamanda Mzee kwa kuiwezesha kuipatia timu ya Tanzania Prisons gari ambalo litawasaidia katika safari kwenye michezo mbalimbali ikiwemo ya Ligi Kuu,” alisema Matrida.
Aidha Matrida aliongezea kuwa wanaimani kubwa na Jenerali Mzee na wanamini ataisadia klabu hiyo ili iweze kusonga mbele.
Kwa sasa Prisons inashika nafasi ya nane, kwenye msimamo wa Ligi Kuu baada ya kujikusanyia alama 41 baada ya kucheza michezo 30.
Leave a comment