Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania na Afrika Kusini zakumbushia uhusiano
Habari Mchanganyiko

Tanzania na Afrika Kusini zakumbushia uhusiano

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini Tanzania, Elisante Gabriel
Spread the love

SERIKALI ya Afrika Kusini imesema inatambua mchango wa nchi ya Tanzania katika harakati za kuipatia uhuru nchi hiyo kupitia program ya urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika, anaandika Dany Tibason.

Viongozi kutoka nchi hizo mbili wapo mjini Dodoma kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa siku tatu unaojadili  urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini Tanzania, Elisante Gabriel amesema kuwa program hiyo imewakutanisha wataalamu, makatibu wakuu na mawaziri wa wizara mbalimbali zilizoshiriki katika vita vya ukombozi kutoka nchi hizo mbili kwa lengo la  kuweka uelewano wa pamoja

“Lakini jambo lingine kubwa ni kwamba tunapenda kuweka historia vizuri ili hata vizazi vijavyo vitambue mchango wa Tanzania katika ukombozi wa Bara la Afrika ilikuwaje, na pia tufikie hatua ambapo kumbukumbu hizo ziwekwe kwenye mfumo wa kidigiti ambayo itatuzwa kwa muda mrefu zaidi” amesema Elisante.

Mkurugenzi mkuu wizara ya ujenzi nchini Afrika Kusini Mziwoke Dlabantu amesema kuwa nchi yao inatambua kazi kubwa ambayo imefanywa na Tanzania katika vita ya ukombozi wa nchi hiyo.

Washiriki wa mkutano  huo watatembelea makaburi ya wapigania uhuru yaliyopo wilaya ya Kongwa iliyopo mkoani Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!