Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tamasha la utamaduni kufanyika Dar
Habari Mchanganyiko

Tamasha la utamaduni kufanyika Dar

Kijiji cha Makumbusho
Spread the love

KAMPUNI ya masoko inayojishughulisha na ushauri na mikakati kwa wateja ZECHY Afrika imeandaa tamasha la kusheherekea utamaduni wa mtanzania (Chemichemi Canival) litakalofanyika mwezi Septemba katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar Es Salaam, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Lena Kimani mratibu wa tamasha amesema: “Tamasha la chemichemi linatarajia kuzinduliwa kwa kusherehekea utamaduni wa Mtanzania. Kuna matamasha mengi nchini lakini hili linalenga kusherehekea utamaduni wetu.”

Akiendelea kuongea amesema kwamba wameona uhitaji wa kufanya tamasha hilo ili kuwasaidia wanaoishi mjini kuzifahamu na kujifunza kwa ukaribu tamaduni zao kwani wengi wao hawana ukaribu na vijijini wanakotoka hali inayofamya vijana kuwa na maana hasi kuhusu utamaduni wao.

“kutokana na utandawazi mwenendo wa maisha ya watanzania wanaoishi mjini wemgi wao hawana ukaribu na vijijini wanakotoka na hili limefanya vijana wengi wa sasa kuwa na nana hasi kuhusu utamaduni wao,” anasema Lena.

Zech wanasema kuwa tamasha hilo litafanyika mara mbili kwa mwaka na hakutakuwa na kiingilio chochote ila wametoa wito kwa watakao hudhulia kuvalia nguo zao za asili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!