Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari
Habari za SiasaTangulizi

Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Spread the love

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemugeuzia kibao Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  (Chadema)  ambaye amewapelekea ushahidi wa namna Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alivyotumia rushwa kuwashawishi Madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukihama chama hicho, anaandika mwandishi wetu.

Tofauti na ilivyotarajiwa na wengi kwamba  taasisi hiyo ingeufanyia kazi ushahidi uliowasilishwa kwao na Mbunge huyo, lakini leo imemuonya mwanasiasa huyo na kumtaka asitoe aina yoyote ya shinikizo baada ya kuwapa ushahidi.

“Hii Taasisi haishinikizwi na mtu yeyote na hapaswi hata mara moja kutushinikiza…. natoa onyo jingine, endapo ataendelea na utaratibu huu tutachukua hatua za kisheria dhidi  yake”

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola, ametoa onyo hilo leo na kusisitiza kuwa hawafanyi kazi kwa shinikizo la mtu.

Nassari akiongozana na wabunge kadhaa wa Chadema wameiwasilisha ushahidi huo wa video kwa TAKUKURU ili iweze kufanya uchunguzi wake kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!