Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Takukuru yamhoji Sethi
Habari Mchanganyiko

Takukuru yamhoji Sethi

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 8 Novemba 2018 imeelezwa kwamba mtuhumiwa katika kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi amechukuliwa maelezo yake na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Takukuru, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ameieleza mahakama hiyo kuwa, jana walifanikiwa kuchukua maelezo ya Sethi.

Wakili Swai ameieleza mahakama kuwa, baada ya Takukuru kuchukua maelezo ya Sethi, wanaendelea na hatua za upelelezi zinazofuata.

Kufuatia kauli hiyo, Wakili wa Sethi, David Chillo aliutaka upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu Shaidi kutokana na maelezo ya pande zote mbili, aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 22 Novemba 2018, siku ambayo tarehe itakapotajwa, pamoja na kuangalia kama upelelezi umekamilika au bado.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!