Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru) imeshindwa kuwahoji viongozi waandamizi wa Chama cha ACT-Wazalendo, kwa kile kilichodaiwa kuwa Ofisa aliyetakiwa kuwahoji hayupo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi wa ACT-Wazalendo ambao walitakiwa kuhojiwa ni Ado Shaibu Katibu  wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho na Dorothy Temu, Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Leo Tarehe 25 Juni  2019,  viongozi hao waliitwa makao makuu ya Ofisi za Takukuru yaliyokuwepo Upanga jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Viongozi hao waliwasili kwenye Ofisi za Takukuru saa 7 na robo mchana na baadaye saa 8 kamili walielekea ghorofa ya juu kwa ajili ya kusikiliza wito wao ambapo waliambiwa kuwa Ofisa aliyewaita hayupo hivyo wataitwa siku nyingine.

Ado ameiambia MwanaHALISI ONLINE kuwa hadi wakati huu hawajaambiwa lengo la wito huo lakini kutokana na chama chao kimekuwa kikiubua mijadala mbalimbali inayohusu uchumi wa nchi inawezekana ikiwa ni moja ya sababu ya taasisi hiyo kuwaita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

error: Content is protected !!