JESHI la Polisi Singida Mjini limemnyika dhamana Mbunge wa zamani wa Jimbo la Singida Kaskazini na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na wenzake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).
Nyalandu leo mapema alishikiriwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Singida kwa mahojiano pamoja na David Jumbe na Samson ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema, Kata ya Itaja.
Kwa mujihu wa taarifa iliyotolewa na Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chadema, inasema baada ya mahojiano TAKUKURU walimua kuwaachia Nyalandu na wenzake lakini Jeshi la Polisi waliwashikiria kwa mahojiano zaidi.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa baada ya Polisi kumaliza kuwahoji na kuandikisha maelezo waliruhusiwa kwa dhamana, lakini ghafla OCD akabadili uamuzi akidai amepokea maelekezo.
@takukuru_tz Singida walikopelekwa awali, baada ya kuwahoji waliwakabidhi kwa @tanpol Singida mjini, ambako walipomaliza kuandikisha maelezo waliruhusiwa kwa dhamana, ghafla OCD akabadili uamuzi akidai amepokea maelekezo @JamiiForums @VOANews @iddligongo @bbcswahili @dwnews
— Tumaini Makene (@McCainTumaini) May 27, 2019
Leave a comment