Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars kibaruani CHAN dhidi ya Zambia
Michezo

Taifa Stars kibaruani CHAN dhidi ya Zambia

Spread the love

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ leo kwa mara ya kwanza itashuka dimbani dhidi ya Zambia, katika michuano ya kombe la mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani inayofanyika Cameroon. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa kundi D, utachezwa majira ya saa 1 usiku kwenye Uwanja wa Omnisports uliopo kwenye mji wa Limbe, Cameroon

Hii itakuwa mara ya pili kwa timu hizo kukutana kwenye michuano hiyo wakiwa kwenye kundi moja kama ilivyotokea mwaka 2009 ambapo Stars ilifuzu kwenye michuano hiyo ikiwa chini ya kocha Raia wa Brazil, Marcio Maximo.

Kuelekea kwenye mchezo huo huenda kocha wa Taifa Stars, Ettiene Ndayiragije akakosa huduma ya mshambuliaji wake John Bocco kutokana na kuwa na majeruhi ambayo aliyapata toka akiwa na klabu yake ya Simba licha ya kujumuishwa kwenye kikosi hiko.

Taifa Stars inahitaji ushindi kwenye mchezo huu wa leo ili kujiwekea mazingira mazuri ya kufuzu kwenye hatau ya robo fainali ya michuano hiyo.

Kwenye kundi hilo Stars yupo pamoja na timu za Mali, Zambia na Guinea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!