VIRUSI vya Corona vinaendeleo kuitesa dunia, tayai imesababisha madhara makubwa katika nchi mbalimbali duniani. Anaandika James Iyambogo, Mwanza … (endelea).
Ugonjwa huo husambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine au mnyama kwenda kwa binadamu.
Tayari virusi vya Corona vimesambaa zaidi ya nchi 50 duniani, virusi hivyo vilianza kuishambuliwa China. Zaidi ya watu 4000 wamepoteza maisha hadi sasa. Barani Afrika, virusi hivyo vimebisha hodi.
Nchini Tanzania virusi hivyo bado havijaripotiwa kwepo, hata hivyo serikali imetoa tahadhari sambamba na kutoa elimu kuhusu ugonjwa huo hatari.
Njia zinazotumika kuambukiza Corona:
Kugusana na mgonjwa, kujigusa mikono machoni, mdomoni bila kunawa mikono, kugusa kitu ama sehemu aliyoguswa na mgonjwa vyote hivi vinaweza kukusababishia kupata maabukizi ya virusi vya Corona.
Dalili
Homa kali na mafua, kuumwa kichwa, mwili kuchoka, kukohoa, kubanwa mbavu, maumivu ya misuli, vidonda vya koo na kupumua kwa shida hizi na nyingine ni ukiona hivyo fika mara moja hospitali, na epuka kumshika mtu wa namna hiyo.
Namna ya kujikinga, zigatia usafi binafsi, kufunika mdomo na pua wakati wa kukohoa kwa kutumia ‘Tissue’, epuka kushikana mikono na mtu mwenye historia ya kusafiri nje ya nchi kwa sasa, epuka kugusana na mgonjwa mwenye dalili za magonjwa piga simu. haraka hospitali, chukua taadhari unapopokea mgeni kutoka nje ya nchi kwa kutoa taarifa na kumpeleka hospitali.
Leave a comment