Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sunflag: Tumeongeza ufanisi, tupeni kazi
Habari Mchanganyiko

Sunflag: Tumeongeza ufanisi, tupeni kazi

Wafanyakazi wa kiwanda cha Sunflag kilichopo eneo la Themi jiji la Arusha wakiendelea na uzalishaji wa nguo za aina mbalimbali
Spread the love

UONGOZI wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguo cha Sunflag, kilichopo mkoani Arusha, kimeeleza kuwa na uwezo wa kuzalisha sare za majeshi na shule nchini baada ya kuongeza uwezo, mitambo na ujuzi wa wataalamu wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Haroun Mahundi, meneja uzalishaji wa kiwanda hicho amemweleza Angellah Kairuki, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia uwekezaji.

Amesema, awali walipewa zabuni za kutengeneza sare hizo lakini baadaye ziliondolewa bila taarifa na kwamba, kiwanda hicho katika miaka ya hivi karibuni, kimeongeza uwezo maradufu wa uzalishaji kuanzia hatua ya kutengeneza nyuzi kwa kutumia pamba, vitambaa vya aina mbalimbali na nguo zinazouzwa ndani na nje ya nchi.

“Tuna uwezo wa kutengeneza nguo za aina mbalimbali na sare kwa majeshi yote kwa viwango vya juu, ni vizuri kiwanda hiki kitumike kikamilifu kuipunguzia serikali gharama ya kuagiza nje ya nchi,” amesema Mahundi.

Waziri Kairuki baada ya kutembelea idara mbalimbali za kiwanda hicho, aliridhishwa na uwezo wake na kuahidi serikali ipo tayari kushirikiana na mwekezaji kutatua changamoto zinazowakabili ili kuongeza tija.

Amesema, mpango wa Serikali ya Awamu ya tano ni kujadiliana na wawekezaji ili kushughulikia changamoto zinakwamisha uwekezaji katika maeneo mengi, ikiwemo sekta ya viwanda ambayo inatoa ajira kwa vijana wengi na kuitangaza nchi kupitia bidhaa zinazozalishwa.

Amesema, hatua ya asilimia 50 ya nguo zinazozalishwa, kuuzwa nchini ni mafanikio muhimu yanayoonesha wananchi kwamba wamejenga utamaduni wa kununua bidhaa zenye viwango vya juu kutokana na uchumi kuimarika.

Amesema, siku za nyuma asilimia 70 ya nguo zilikua zikiuzwa nje ya nchi huku 30 ikibaki nchini.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!