Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sumaye, Kubenea wapeta Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Sumaye, Kubenea wapeta Chadema

Frederick Sumaye, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema. Picha ndogo, Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

FREDERICK Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu wa serikali ya awamu ya tatu na Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo wameibuka nafasi tofauti za uongozi wa Chadema Kanda ya Pwani walizokuwa wakiwania, anaandika Charles William.

Sumaye alikuwa akiwania nafasi ya mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, huku Kubenea akiwania kuwa makamu mwenyekiti wa kanda hiyo.

Uchaguzi huo ambao wapiga kura wake ni wajumbe wa mkutano maalum wa Baraza la Uongozi Kanda ya Pwani umefanyi Jumapili, Machi 19, katika ukumbi wa Lamada Hotel, jijini Dar es Salaam.

Sumaye ameibuka na ushindi wa kura 74 sawa na asilimia 83 huku mpinzani wake pekee Gango Kidera akipata kura 15 sawa na asilimia 17.

Katika nafasi ya makamu mwenyekiti wa kanda hiyo, Kubenea ameshinda kwa kura 60 sawa na asilimia 67.41, Mustafa Hassanali kura 18 sawa na asilimia 20.2 huku Adolf Mkono akipata kura 11 sawa na asilimia 12.35.

Kwa upande wa nafasi ya mweka hazina, Ruth Mollel ameibuka na ushindi wa kura 50 dhidi ya Lucy Magereli aliyepata kura 20 (mbunge wa viti maalum pia) huku Florence Kasilima akiambulia kura 19.

Idadi ya wapiga kura waliotakiwa kushiriki uchaguzi huo ni 112 lakini waliojitokeza ukumbini na kipiga kura ni 89.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!