Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sugu, Masonga wahukumiwa miezi mitano jela
Habari za SiasaTangulizi

Sugu, Masonga wahukumiwa miezi mitano jela

Joseph Mbilinyi 'Sugu' akiwa mahakamani akisikiliza hukumu yake
Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (SUGU) na Emmanuel Masonga, Katibu wa Kanda ya Nyasa Chadema, wamehukumiwa kwenda jela miezi mitano kwa kosa la uchochezi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite, baada ya kujiridhisha kuwa watuhumiwa hao wana hatia dhidi ya kesi ya kutumia lugha ya fedheha kwa Rais John Magufuli

Sugu pamoja na Masonga walifikishwa mahakamani hapo kwa mara kwanza Januari 19, 2018, kwa kosa hilo walitoa kauli hizo katika mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana wakiwa viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Maneno yaliyomtia hatiani Sugu na mwenzake ni “Mhe Rais Magufuli hawezi kupendwa na watu kwa kumshoot risasi Lissu, kumtupa Jela miezi minne Lema, kumteka Ben saanane, kumteka Roma na kumzuia SUGU asiongee.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!