Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Sugu achomoka kwa dhamana, kutinga polisi leo
Habari Mchanganyiko

Sugu achomoka kwa dhamana, kutinga polisi leo

Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu)-Chadema jana jioni alifanikiwa kupata dhamana baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya asubuhi ya siku hiyo kwa madai ya uchochezi. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Sugu alifika kituoni hapa jana asubuhi akiitikia wito wa jeshi hilo uliomtaka kufanyi hivyo kwa madai ya kukashifu mamlaka za serikali hususani kukejeli ugawaji wa vitambulisho vya mjasiriamali.

Mbunge huyo alipifika kwenye Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu video unayosambaa akionekana ‘kukejeli’ mamlaka za serikali, alizuiwa kutoka.

Sugu anadaiwa kutoa kauli hiyo alipozungumza na wananchi wakati akitoa msaada katika Shule ya Msingi Ikuti, Mbeya. Hata hivyo, Jeshi la Polisi mkoani humo lilimpa dhamana majira ya saa 1 jioni baada ya kuwekewa dhamana ya bondi ya Sh 5 milioni. L anatakiwa kwenda kuripoti kituoni hapo.

Urich Matei, Makanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema, kuwa kesi ya Sugu ni ya uchochezi na kwamba, amepewa dhamana huku uchunguzi ukiendela.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!