REBECCA Kadaga, Spika wa Bunge la Uganda amemwandikia barua Rais Yoweri Museveni akimtaka kuhakikisha kwamba, polisi waliohusika kumpiga na kumjeruhi, Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine,’ Mbunge wa Kyadondo wanachukuliwa hatua. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Spika Kadaga ametaka polisi hao wanaodaiwa kuwa baadhi yao ni walinzi wa Rais wa Museveni wanakamatwa mara moja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.
Kassiano Wadri, miongoni mwa wanasiasa waliowekwa kizuizini na Bobi Wine alidai kuwa Mbunge huyo wa Kyadondo alipigwa mara kwa mara na walinzi wa rais ambapo baadhi yao walikuwa wameficha nyuso zao.
Hata hivyo, serikali ya Rais Museveni imekanusha madai hayo ikisema kuwa ni ya uongo.
Leave a comment