Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai leo Jumanne tarehe 15 Desemba 2020, atawaapisha wabunge wanne wa ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imesema, wabunge hao wataapisha saa 10 jioni katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020, ACT-Wazalendo kilishinda majimbo manne ya Pemba visiwani Zanzibar.

Walioshinda ni; Hatibu Said Haji (Konde), Salum Mhamed Shafi (Chonga), Omar Ali Omar (Wete) na Khalifa Mhamed Issa wa Mtambwe.

Wabunge wateule wanakwenda kuapishwa baada ya chama hicho kuwaruhusu wanachama wake wote walioshinda udiwani, ubunge na uwakilishi kwenda vyombo vya uwakilishi ili kuapishwa na kuanza kuwatumikia wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!