Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai azuia wakurugenzi wa Uchaguzi kuguswa
Habari za Siasa

Spika Ndugai azuia wakurugenzi wa Uchaguzi kuguswa

Spread the love

SPIKA wa Bunge Job Ndugai amemzuia Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Susan Kolimba kujibu maswali ya Mbunge wa Kitambile Masoud Abdallah Salim ambapo mojawapo lilihoji kuwa, lini serikali itapeleka mswada bungeni wa kubadili sheria inayoruhusu Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Salim aliuliza amswali hayo leo tarehe 13 Septemba 2018 bungeni jijini Dodoma, ambapo amedai kuwa, kitendo cha wakurugenzi wa halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi, kinaminya uhuru wa demokrasia kutokana kwamba wakurugenzi hao ni makada wa chama tawala nchini CCM na hivyo ikifika kipindi cha uchaguzi wanakuwa marefa wa kuisaidia CCM kupata ushindi.

Mbunge huyo alilielekeza maswali mawili ya nyongeza katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambapo swali lilingine aliihoji wizara hiyo kwamba, kwa nini serikali imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei ya sukari kitendo kinachochangia ugumu wa maisha kwa wananchi.

Baada ya Salim kuuliza maswali hayo, Spika Ndugai aliyakataa maswali hayo akisema kuwa hayaendani na swali lake la msingi pamoja na kuuliza katika wizara isiyo sahihi, lakini pia kuhusu swali lake mfumuko wa bei ya sukari, alisema litajibiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!