Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai awanyoosha wapinzani bungeni, akiilinda mahakama
Habari za Siasa

Spika Ndugai awanyoosha wapinzani bungeni, akiilinda mahakama

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge, amezuia Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Katiba na Sheria kusomwa bungeni jijini Dodoma, kwa maelezo kwamba inashambulia Mhimili wa Mahakama. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hotuba hiyo ilitakiwa kusomwa bungeni hapo, jana tarehe 17 Aprili 2020, katika mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi, ya wizara ya katiba na sheria kwa mwaka wa fedha wa 2020/21.

Spika Ndugai amedai kuwa, hotuba hiyo imeandikwa kwa kutumia lugha inayotweza mhimili wa mahakama.

“Kubwa zaidi linalonisumbua, tumesisitiza si vizuri mhimili wa bunge kuwa kituo cha kushambulia mahakama. Kuanzia kifungu cha 66, 67, 68, 69, 70, 71, 72 na 74. Kila pahali pamekuwa na lugha ambayo ni ya kutweza mahakama. Kuonesha Mahakama ya Tanzania si chochote haipendezi,” ameeleza Spika Ndugai.

Sababu nyingine aliyotoa Spika Ndugai iliyopelekea kuzuia hotuba hiyo kusomwa bungeni, ni kutojikita katika mjadala wa upitishwaji wa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo, kwa mwaka ujao wa fedha.

“Tuanze kwanza ni nini madhumuni ya ya kikao hiki, madhumuni ni waziri wa katiba na sheria amewasilisha hoja mbele yetu. Bunge likubali kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya katiba na sheria, kwa mwaka wa fedha wa 2020/21. Hotuba hii kuanzia ukurasa wa kwanza hadi wa mwisho haijagusa bajeti hii,” amesema Spika Ndugai na kuongeza:

“Hakuna mahali inaonyesha bajeti hii.  Inaonekana kama imeandikwa na watu fulani mahali ambao hawajui nini kinaendelea bungeni.”

Aidha, Spika Ndugai amesema kama kambi hiyo haitarekebisha makosa hayo, hatosita kuzuia hotuba zake kusomwa bungeni.

Hii ni mara ya pili kwa Spika Ndugai kuzuia hotuba ya kambi rasmi ya upinzani kusomwa bungeni, ambapo mara ya kwanza alizuia hotuba kuhusu Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Bado meza ina shida na hotuba za kambi rasmi ya upinzani bungeni, na kama nilivyoanza na ofisi ya waziri mkuu, tusipotafuta namna ya kurekebisha hilo tatizo, basi itabidi twende hivyo hivyo maana mtakuwa mmechagua wenyewe,” amesisitiza Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!