Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 
Habari za Siasa

Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ametangaza kusitisha kutoa karatasi zinazoonesha orodha ya vikao vya shughuli za Bunge. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Septemba 2019 wakati akitoa tangazo kwa wabunge na kueleza, katarasi hizo hazitatumika tena ndani ya ukumbi wa Bunge na badala yake watakuwa wanatumia njia ya kimtandao.

Na kwamba, wabunge watakuwa wakipewa orodha ya shughuli za Bunge kwa kutumia njia ya mtandao.

“Nataka kuwaambia wabunge kuwa katarasi hizi ambazo tunazitumia kama kuonesha orodha ya shughuli za Bunge, leo ndio siku ya mwisho kungia humu ndani.

“Tunaanza na karatasi hizi na kwa maana nyingine tutakuwa tunawatumia kwa njia ya mtandao, sasa waheshimiwa wabunge naomba mhakikishe mnaweka namba zenu za simu vizuri, barua pepe vizuri na lengo ni kuhakikisha meza za wabunge haikai na makaratasi na badala yake zinakuwa nyeupe kabisa,” amesema Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!