Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai aimwagia sifa Kenya
Habari za SiasaKimataifa

Spika Ndugai aimwagia sifa Kenya

Bunge la Kenya
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ameipongeza Kenya kwa kuzindua Kanuni za Kudumu za Bunge lake, kwa lugha ya Kiswahili. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Spika Ndugai ametoa pongezi hizo leo tarehe 31 Oktoba 2019, wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, nchini Kenya.

Aidha, Spika Ndugai amelipongeza Bunge la Kenya kwa hatua ya kuanzisha utaratibu wa kurusha moja kwa moja, matangazo ya vikao vya kamati mbalimbali.

“Nawapongeza kwa uzinduzi, kwamba sasa vikao vya kamati mbalimbali vitapeperushwa mubashara,” amepongeza Spika Ndugai.

Pia amezitaka nchi za Afrika Mashariki kutumia lugha ya Kiswahili katika vikao vyake vya Bunge.

“Nchi zetu kwa muda mrefu zimefunikwa na kasumba ya kuamini kwamba, lugha zetu ni dhaifu na za watawala wetu ni lugha za juu.

“Hatuna sababu za kuwa wanyonge kwa kutumia kiswahili bungeni,” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!