Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Solskjaer ampigia chapuo Greenwood England
Michezo

Solskjaer ampigia chapuo Greenwood England

Spread the love

Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amempigia debe kinda wake, Mason Greewood katika kikosi cha timu ya Taifa ya England, kutokana na kiwango alichokionyesha kwa hivi karibuni. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Greenwood ambaye mwenye umri wa miaka 18, hivi karibuni amekuwa na kiwango kizuri kwa kufanikiwa kufunga mabao matatu kwenye michezo dhidi ya Bournemouth na Brighton yote ya Ligi Kuu nchini England.

Kocha huyu amesema kuwa kama mchezaji huyo anaweza kumudu kucheza ndani ya Manchester United basi pia ataweza kucheza kwenye klabu na timu yoyote kwa sababu ana ubora ambao wengine hawana.

“Anaweza kucheza kwenye timu ya wakubwa England au hata chini ya miaka 21, mimi sitajali, najua anafanya vizuri kwetu na jambo kubwa kuwa naye,” alisema kocha huyo.

“Kama ameweza kumudu kucheza Manchester United kwa hiyo anaweza kumudu kucheza timu yoyote na Mason anaubora ambao wengine hawana,” aliongezea Solskjaer.

Greenwood ambaye amelelewa kwenye kituo cha Manchester United mpaka sasa ameshacheza michezo 29 ya Ligi Kuu England, na kufunga jumla ya mabao nane toka alipopandishwa kwenye timu ya wakubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!