Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sirro abadilisha makamanda wa polisi
Habari Mchanganyiko

Sirro abadilisha makamanda wa polisi

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi katika maeneo kadhaa, anaandika Catherine Kayombo.

Miongoni mwa waliobadilishwa vituo vya kazi ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ambaye amepelekwa kuwa Mkuu wa Kitengo cha Mafao na Fidia, makao makuu ya polisi.

Nafasi ya Kaganda imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Murilo Jumanne Murilo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga.

Aliyeteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ni Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Haule, aliyekuwa afisa mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa leo na Msemaji wa Polisi, Barnabas Mwakalukwa, mabadiliko hayo ni ya kawaida ndani ya jeshi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!