Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sinema ya Lissu na Polisi yaendelea Dar
Habari za SiasaTangulizi

Sinema ya Lissu na Polisi yaendelea Dar

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, akiwa chini ya ulinzi wa polisi
Spread the love

JESHI la polisi limeendelea kumshikilia Mwanasheria mkuu wa Chama cha Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu aliyekamatwa juzi jijini Dar es Salaam na kushikiliwa katika kituo kikuu, anaandika Hellen Sisya.

Mwanasheria huyo leo alitarajiwa kupelekwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka yake, lakini mpaka sasa hajapelekwa huko.

Tumaini Makene, Ofisa habari wa chama hicho, amesema kwamba chama hicho kinatarajia kwamba mwanasheria huyo atapata dhamana ya polisi na kwamba hilo lisipofanyika watachukua hatua za kisheria kuhusiana na hilo.

Mpaka sasa haijulikani hatma ya Lissu japokuwa Chadema bado wanaendelea kutoa taarifa za matumaini kwamba huenda leo mwanasiasa huyo anaweza kupata dhamana ama polisi au mahakamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!