Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yatangaza michuano yake, kocha mpya…
MichezoTangulizi

Simba yatangaza michuano yake, kocha mpya…

Barbara Gonzalez, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba
Spread the love

 

TIMU ya Simba ya Dar es Salaam, imetangaza michuano ya Kimataifa ‘Simba Super CUP’ ikihusisha timu tatu Simba, TP Mazembe ya Congo na Al Hilal ya Sudan. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Pia, timu hiyo imesema, kesho Jumamosi, itamtangaza kocha mpya atakayechukua mikoba ya Sven Vanderbroeck aliyeondoka. Kocha mpya atasaidiwa na kocha msaidizi, Suleiman Matola.

Akitangaza michuano hiyo leo Ijumaa tarehe 22 Januari 2021, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba (CEO), Barbara Gonzalez amesema, michuano hiyo, itaanza Jumatano ijayo tarehe 27- 31 Januari 2021.

Amesema, mechi ya kwanza itakuwa Simba dhidi ya Al Hilal saa 11 jioni.

Haji Manara, Ofisa Habari wa Klabu ya Simba

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema, michuano hiyo “ni maalum kwa mabingwa wa nchi, kama timu yako siyo bingwa, huhusiki na michuano hii.”

“Lakini, michuano hii ni maalum kwa maandalizi ya michuano ya klabu bingwa, tunataka kushinda kikombe,” amesema Manara

Amesema, kabla ya michuano hiyo kuanza, benchi lote la ufundi litakuwa limekamilika na “kuanzia kesho, tutaanza kutangaza kocha na benchi lake la Ufundi.”

“Ndani ya siku mbili au tatu zijazo, tutakuwa na kocha mkuu mpya atakayesaidiana na Suleiman Matola,” amesema Manara

Manara amesema, “malengo yetu kimataifa ni kufikia nusu fainali, lakini malengo yetu mama ni kushinda ligi kuu na kombe la FA.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!