Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yasajili beki kitasa cha Zimbabwe
Michezo

Simba yasajili beki kitasa cha Zimbabwe

Peter Muduhwa
Spread the love

 

KLABU ya Simba imekamilisha usajili wa beki wa kati, Peter Muduhwa raia wa Zimbabwe ambaye alikuwa kwenye michuano ya kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wandani CHAN na timu yake ya taifa inayoendelea nchini Cameroon. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam  …(endelea).

Mchezaji huyo ambaye alikuwa akichezea klabu ya Highlanders FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Zimbabwe, ametambulishwa na klabu ya Simba leo tarehe 26 Januari 2021, ambapo ataitumikia timu hiyo kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa, baada ya usajili wa ndani kufungwa.

Peter Muduhwa

Muduhwa ambaye ametua nchini leo na kusaini mkataba wa miezi sita na mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Usajili wa mchezaji huyo utaifanya Simba mpaka sasa kuwa imesajili wachezaji watatu kwa jili ya michuano hiyo ambayo kwa sasa wamefikia kwenye hatua ya makundi, ambapo mchezo wa kwanza watacheza tarehe 12 Februari 2021 nchini Congo DR dhidi ya AS Vita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!