Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup
Michezo

Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup

Wachezaji wa Simba na Yanga wakiingia uwanjani katika moja ya pambano lao
Spread the love

HATIMAYE mahasimu wa wawili katika soka la Tanzania, Simba na Yanga wataminyana kesho katika hatua ya nusu fainali kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar baada ya kukamilika kwa michezo ya hatua ya makundi jana.

Simba wanakutana na Yanga baada ya kufanikiwa kumaliza vinara katika kundi A huku nafasi ya pili ikishikwa na timu ya Taifa Jang’ombe ambao walifanikiwa kupata ushindi jana mbele ya mabingwa watetezi URA kutoka nchini Uganda.

Katika mchezo huo utakaopigwa kesho majira ya Saa 2:15 usiku Yanga inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kataika mchezo uliomalizika dhidi ya Azam FC baada ya kupata kipigo cha mabao 4-0.

Mchezo wa pili wa nusu fainali utaikutanisha klabu ya Azam FC dhidi ya timu ya Taifa Jang’ombe ambayo ndio timu pekee kutoka visiwani humo kufikia hatua hiyo katika michuano hiyo inayotalajia kukamilika tarehe 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!