Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba wang’ara tuzo za mwezi VPL
Michezo

Simba wang’ara tuzo za mwezi VPL

Spread the love

KOCHA mkuu wa klabu ya Simba Patrick Aussems na mshambuliaji wake, Miraji Athuman wameibuka vinara wa tuzo za mwezi Septemba za Ligi Kuu Tanzania Bara 2019/20. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Miraji amefanikiwa kushinda tuzo hiyo baada ya kumshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi, baada ya kuwashinda mwenzake wa klabu ya Simba Meddy Kagere na Ismail Kada kutoka Tanzania Prisons, wakati Aussems ameshinda tuzo ya kocha bora baada ya kuwabwaga makocha Mohammed Rishard wa Prisons na Abdallah Mohammed Baresi wa JKT Tanzania.

Aussems amefanikiwa kushinda tuzo hiyo baada ya kufanikiwa kuingoza Simba kushinda michezo minne ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kufanikiwa kukusanya jumla ya pointi 12 na kufanya timu hiyo kuwa kileleni kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Kwa upande wa Miraji ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwa katika kiwango kizuri kwa kufanikisha timu yake kupata ushindi mbele ya Mtibwa Sugar baada ya kufunga bao la pili sambamba na kutoa pasi mbili za mabao na hivyo atazawadiwa kiasi cha Sh. 1,000,000 kutoka kwa mdhamini wa mkuu wa Ligi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!