Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) sambamba na bodi ya ligi wamekamilisha maandalizi yote kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakao wakutanisha miamba miwili ya soka nchini Simba dhidi ya Yanga, ikiwemo kutoa majina ya waamuzi watakao chezesha mchezo huo sambamba na kutaja viingilio kwenye mchezo huo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)
Makamu M/nyekiti wa bodi ya ligi Ibrahim Mwayelwa ameeleza kuwa mchezo huo ni mkubwa sana kwenye historia ya mpira wa Tanzani kwa kuwa unakusanya idadi kubwa ya mashabiki hivyo wameshaimalisha maswala mbali mbali ikiwamo ulinzi na namna mashabiki watakavyoweza kuingia uwanjani bila usumbufu wowote.
“Asilimia kubwa ya maandalizi yamesha kamilika ikiwamo kutaja waamuzi wa mchezo huo na bado vikao mbalimbali vinafanyika ili kuufanya mchezo huu kuchezwa kwa taratibu na kanuni zinazohitajika ili uweze kumalizika salama” alisema Ibrahim Mwayelwa
Mwayelwa aliongezea kuwa mpaka sasa tiketi za mchezo huo zimesha anza kuuzwa kwa mawakala wote wa Selcom hivyo ametaka mashabiki kununua mapema ili kuepuka usumbufu ambapo tiketi za VIP A zitauzwa kwa shilingi 30000, VIP B na C zitakuwa shilingi 20000 huku mzunguko zitauzwa kwa bei ya shilingi 7000.
Mwamuzi wa kati wa mchezo huo atakuwa Jonesian Rukya (Kagera) huku akisaidiwa na Hamisi Chang’walu na Sudi Lila pamoja na mwamuzi wa akiba Elly Sasii wote kutoka (Dar es Salaam) huku kamishna wa mchezo ni Khalid Bitebo kutoka Mwanza.
Mchezso huo unatarajian kuanza majira ya saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam huku timu zote zikisaka ushindi kujiweka sehemu nzuri kwenye msimamo wa ligi.
Mara ya mwisho zilipokutana timu hizi mbili Yanga ilipoteza mchezo huo kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Simba, bao lilifungwa na mshambuliaji Meddy Kagere kwa njia ya Kichwa akipokea pasi kutoka kwa Johhn Bocco.
Leave a comment