WATU watatu wavuvi katika Ziwa Victoria wilayani Busega, Simiyu wamefariki dunia baada ya mtumbwi wao kupasuka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).
Taarifa kutoka Simiyu zinaeleza, maafa hayo yametokea jana tarehe 29 Novemba 2020, katika Kata ya Kabita wakati wavuvi wao wakiwa kazini.
Richard Abwao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu amewaeleza waandishi wa habari leo tarehe 30 Novemba 2020, kwamba baada ya mtumbwi huo kupasuka, watu hao walikunywa maji mengi pia kukosa hewa jambo lililowasababisha mauti.
Waliotajwa kupoteza maisha ni Mnaga Manyama (28), Kulwa Juma (15) na Bitulo Manyama.
Kamanda Abwao anasema, wawtu hao wote walikuwa wakazi wa Kibata iliyopo kwenye Wilaya ya Busega mkoani humo na kwamba, taratibu zingine zinaendelea.
Leave a comment