ALIYEKUWA mbunge wa Momba kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), DAVID Silinde amechukua fomu ya kugombea ubunge Tunduma Mkoa wa Songwe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Silinde amechukua fomu hizo leo Jumanne tarehe 14 Julai 2020. Hadi mchana, wagombea 16 walikuwa wamekwisha chukua fomu kuwania nafasi hiyo.
Jimbo la Tunduma lilikuwa linaongozwa na Mbunge wa Frank Mwakajoka wa Chadema.
Soma zaidi hapa
David Silinde ajiuzulu
MwanaHALISI Online limezungumza na Silinde ambaye amesema, “nimepokelewa vizuri na uongozi wa wilaya na kupewa fomu” huku akisema Chadema hakiwezi kushinda Tunduma katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
“Mimi kama mwanachama mpya, nitafuata taratibu zote kulingana na katiba, kanuni na mwongozo na ikiwa nitapitishwa au mtu yoyote kati yetu atapitishwa tutamuunga mkono,” amesema Silinde
“Tutaendesha kampeni za kistaarabu. Sisi kama chama tumejiandaa kushinda Tunduma na sioni kama Chadema wakishinda,” amesema Silinde ambaye amekuwa mbunge kwa miaka kumi mfululizo
Kujiamini