Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Shivyawata waomba walimu maalum mashuleni
Habari Mchanganyiko

Shivyawata waomba walimu maalum mashuleni

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

SHIRIKISHO la vyama vya watu wenye ulemavu (SHIVYAWATA) mkoa wa Dodoma limeomba Wizara ya Elimu kuwapeleka walimu wenye taaluma ya elimu maalum kwenye shule zote nchini. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Shirikisho hilo lilisema kuwa shule nyingi hazina walimu wenye ujuzi wa kutoa elimu kwa watu wenye mahitaji maalum jambo ambalo linawafanya watu wenye ulemavu kutofikia mahitaji wanayotarajia kuyapata.

Ombi hilo lilitolewa Wilayani Kondoa mkoani Dodoma, kwenye kongamano la kujadili umuhimu wa kutambua haki kwa watu wenye ulemavu na jinsi ya kupatiwa huduma stahiki.

Akisoma risala kwa Mkuu wa wilaya ya Kondoa, Zezaria Makota kwenye ufunguzi wa kongamano hilo Katibu wa Shirikisho hilo mkoani hapa, Justus Ng’wantalima amesema kuwa kutokuwepo kwa walimu wenye taaluma ya ya utoaji wa elimu mahalumu kwa watu wenye ulemavu kumesababisha elimu ya watoto kushuka kwa kiwango kikubwa kwa upande wao.

“Hali hiyo imekuwa ikiwakosesha wanafunzi hao kutopatiwa elimu stahiki kama ilivyo kwa wengine ambao hawana ulemavu,hivyo haki za msingi za walio wengi uzikosa kwa kuwa walimu wenye sifa hawapangwi kwenye shule hizo.

“Walimu walio wengi hata wale wenye taaluma bado upamgwa kwenye shule za kawaida wakati sifa zao zinatakiwa kufundisha kwenye shule maalumu zenye wanafunzi wenye uhitaji huo wa elimu stahiki ambayo pia ni haki yao ya msing,” amesema.

Katibu huyo amesema kuwa ili kupunguza makali hayo ya kukosa elimu kwa wanafunzi hao kwa upande wa wa halmashauri pia wanatakiwa kutenga bajeti inayokidhi mahitaji katika shule hizo tofauti ilivyo kwa hivi sasa ambapo ni ndogo ukilinganisha na tatizo lililopo.

Amesema kukosa kwa bajeti hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi hao,hata ufaulu kuwa ni mdogo kutokana na walio wengi kutokuwa na vifaa vinavyohitaji kulingana na ulemavu walionao kwa kila mmoja wapo.

Wakizungumza kwa pamoja kwenye ufunguzi wa kongamano hilo Maafisa maendeleo ya jamii wa halmashauri zote mbili ya wilaya na mji, Hadija Abdallah na Latipha Koshuma, walisema kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wanafunzi wote wanapata haki stahiki juu ya elimu.

Hivyo kwa upande wao halmashauri itashirikiana na shirikisho hilo la vyama kwa lengo la kutatua changamoto mbalimbali ili kuboresha elimu na hususa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwa ajili ya kuwapunguzia makali waliyonayo.

Kwa upande wao kaimu wakurugenzi wa halmashauri hizo za mji na wilaya, Archanus Kilaja na Ally Mwinyikombo, walisema kuwa mbali na chanagamoto walizonazo watu hao wenye mahitaji maalum,pia wanakabiliana na ukosefu wa huduma za kiafya katika vituo mbalimbali.

“Ndugu zetu hao tunafahamu kuwa wana chanagamoto mbalimbali kama vile kwenye miundombinu kutokuwa rafiki,ukosefu wa ajira,kubaguliwa na kunyanyaswa na umasikini,hivyo sisi kama halmashauri tutahakikisha tunashieikiana kwa pamoja kutatua kero hizo,” walisema.

Wakizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo ya Kondoa wakurugenzi hao walisema kuwa kwa kushirikiana na serikali itahakikisha inatatua kero walizokuwanazo watu wenye ulemavu ikiwa na kuwashirikisha katika vikao mbalimbali ili waweze kuleta mchango wao kwa ajili ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!