TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemteua John Shibuda wa Ada Tadea kuwa mgombea urais wa Tanzania na Hassan Konde Kijongoo kuwa mgombea mwenza katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Uteuzi wa wagombea hao umefanywa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage.
Jaji Kaijage amefanya uteuzi huo baada ya kujiridhisha Shibuda na Kijogoo wamedhi vigezo.
Shubuda amekuwa mgombea wa tatu kuteuliwa na NEC akitanguliwa na Rais John Pombe Magufuli wa Chgama Cha Mapinduzi (CCM).
Soma zaidi:-
Wa pili kuteuliwa ni Leopard Mahona wa NRA kuwa mgombea urais wa Tanzania na Ally Khamis Hassan kuwa mgombea mwenza.
Vyama vilivyochukua fomu kuwania kuteuliwa kugombea urais ni 17 kati ya 19 vyenye usajiliwa kudumu.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali
Leave a comment