Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar
Habari za Siasa

Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar

Spread the love

SHAMSI Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, amejitokeza kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Mwanasiasa huyo mkongwe, amechukua fomu hiyo leo asubuhi tarehe 18 Juni 2020, katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui.

“Nakishukuru chama changu kwa yote kilichonifanyia kwa muda wote, na kunipa heshma hii kubwa ya kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama chetu cha mapinduzi.

“Nina hakika, watu wengi na wanachama wengi wangetamani sana Mwenyezi Mungu awape fursa hii, wengine watafanikiwa na wengine hawatafanikiwa,” amesema Nahodha muda mfupi baada ya kuchukua fomu.

Nahodha aliyehudumu nafasi ya Waziri Kiongozi katika Serikali ya Zanzibar kwa miaka 10 (2000 – 2010), anakuwa mgombea wa sita akitanguliwa na makada wengine wa chama hicho ambao ni Hussein Ali Mwinyi, Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi, Omar Sheha Mussa na Balozi Ali Karume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!