Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Shambulio la makombora ya Urusi laua 53
Kimataifa

Shambulio la makombora ya Urusi laua 53

Spread the love

RAIA 53 wameuawa katika shambulio la kombora la Urusi katika kijiji kilichopo mashariki mwa Syria Al-Shafah, kundi la uangalizi linasema.

Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu Syria lililo na makao yake Uingereza (SOHR) linasema 21 kati ya wanaoripotiwa kuuawa Jumapili ni watoto.

Kijiji hicho kipo Deir al-Zour, mojawapo ya majimbo ya mwisho ambako wangambo wa Islamic State wanendelea kudhibiti ardhi.

Awali SOHR lilisema watu 34 wameuawa katika makombora yaliolenga makaazi ya watu. “Idadi hiyo imeongezeka baada ya kuondolewa kifusi baada ya operesheni ya siku nzima ya uokozi,” Rami Abdel Rahman amesema.

Awali Urusi ilithibitisha kwamba walipuaji wasita wa mabomu ya masafa marefu walitekeleza mashambulio ya angani katika eneo hilo, lakini ikasema iliwalenga wanamgambo na ngome zao.

Urusi ni mshirika wa karibu wa rais wa Syria Bashar al-Assad katika vita vya muda mrefu vya kiraia nchini humo.

Mazungumzo ya amani yanayoungwamkono na Umoja wamataifa yanatarajiwa kuanza upya Geneva wiki ijayo, lakini awamu kadhaa za mazungumzo hayakufuwa dafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!