Katibu mkuu wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania Tff, Wilfred Kidau ametoa pole kwa familia ya shabiki mmoja aliepoteza maisha kwenye mchezo wa kufuzu kombe la Dunia 2022 kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania dhidi ya Burundi, kwa mshituko wa moyo baada ya Burundi kusawazisha bao katika kipindi cha kwanza. Anaripoti Martin Kamote… (endelea)
Kidau ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam na kusema kuwa ‘ni mtu ambae ni shujaa na mara baada ya mkutano huu na wandishi wa habari kuisha, nitatoa maelekezo ofisini wanitafutie hio familia inapokaa angalau kama tff tutaenda kujumuika na wenzetu kwenye kipindi hiki kigumu, mtu ambae ametangulia mbele za haki akiwa kwenye kulipigania taifa ni jambo kubwa sana na sisi tuwape pole,
Aidha ameongeza kwa kumpongeza haji manara kwa kazi kubwa alioifanya chini ya kamati yake ya hamasa ambayo ni kamati ndogo ya ushindi wa taifa stars , alifanya jambo kubwa akiwa na wasanii mbalimbali kuelekea kwenye mechi hii na kamati kubwa ya saidia taifa stars ishinde inayoongozwa na mwenyekiti ambae ni mkuu wa mkoa wa dar es salaam paul makonda
Pia ameipongeza serikali kupitia wizara yenye dhamana ya michezo na mhe waziri mwenyewe dkt halson mwakiyembe kwa kazi kubwa.
Tazama video kamili hapo chini
Leave a comment