Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yazindua mpango wa Jiji la Dar es Salaam
Habari za Siasa

Serikali yazindua mpango wa Jiji la Dar es Salaam

Spread the love

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amezindua Master Plan (Mpango Mji) wa jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mpango huo utakaotumika kwa kipindi cha miaka 20 ijayo, umezinduliwa leo Ijumaa, terehe 27 Julai; unalenga kuwapa wadau fursa ya kutoa mapendekezo bora ya jinsi ya kuutekeleza.

Kwa sasa, jiji la Dar es Salaam linatumia master plan iliyoandaliwa mwaka 1979 na ambayo muda wake umeisha mwaka 1999.

Akizungumza na wadau wa jiji la Dar es Salaam, waziri Lukuvi amesema, mpango huo hauna lengo la kuvunja makazi ya watu wakati wa utekelezaji, lakini ametaka waananchi kutonunua maeneo wala kuendeleza ujenzi bila kuwasiliana na wataalamu wa ardhi.

“Ukinunua eneo bila kuwasiliana na wataalamu wa ardhi, unaweza kujikuta unaingizwa mjini. Hii ni kutokana na ukweli kuwa unaweza kununua eneo kwa ajili ya kujenga baa, wakati eneo hilo limetengwa kwa ajili ya shule,” ameeleza.

Ameongeza, “kwa hiyo, mapendekezo haya yasiwashtue. Mpango huu ukianza kutumika, utataka kila kitakachojengwa, kifuate mpango ulivyo.”

Amesema mpango huo ulianza kuandaliwa tangu mwaka 2012, lakini ulicheleweshwa kwa sababu mbalimbali ikiwamo upigaji wa picha za uchambuzi zinazoonyesha kila eneo, hali halisi ya ukuaji wa jiji na dira ya jiji kuwa endelevu.

Wakati huo huo, Lukuvi amepiga marufuku urasimishaji holela wa ardhi kwa dhumuni la kuzidhibiti kampuni za kitapali zilizojitokeza.

Lukuvi ameeleza kuwa utaratibu wa kulipa fedha kwa kampuni zinazoibuka mitaani na kupewa tenda bila kufuata utaratibu na kupitishwa na wataalamu wa ardhi kutoka wilayani.

Amesema, amepata taarifa kuwepo kampuni tatu zilizoibuka kama warasimishaji bila kufuata utaratibu hatimaye walitokomea na pesa za wananchi.

Amesema, ili kuepuka utapeli huo, waziri Lukuvi amepiga marufuku kwa viongozi wa kata na mitaa kuruhusu tenda kwa kampuni zisizopitia ngazi ya wilaya kwa ajili ya kushindanishwa na kuridhiwa kuwa wanasifa ya kurasimisha makazi.

Ameagiza kuwa gharama za upimaji na urasmishaji wa makazi hazitazidi Sh. 250,000 (laki mbili na nusu).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!