SERIKALI imewasiliasha hoja 10 kesi ya kupinga Muswa wa Sheria ya vyama vya siasa iliyofunguliwa na Zitto Kabwe Kiongozi wa ACT-Wazalendo wa Wenzake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Waombaji wengine ni Joran Bashange Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wanachi (CUF) Bara na Salim Biman Mkuregenzi wa Mawasiliano ya Umma (CUF).
Moja ya hoja zilizowasilishwa na serikali kuwa Katiba ya Nchi imegawa mamlaka na kuyaheshimu.
Akiongoza jopo la Mawakili , Wakili Mkuu wa Serikali Mark Mulwambo mbele ya Jaji Benhajo Masoud ameeleza kuwa muhimuli wa Mahakama hauwezi kuingilia Muhimili wa Bunge katika kujadilia mambo yake.
Wakili ameleza kuwa amahakama inaweza kujadili sheria iliyotungwa na Bunge sio muswada ambao haujapitishwa kuwe sheria.
Hoja nyengine ya Serikali ni kwamba waombaji wamewasilisha maombi yao kwa kiapi chenye udhaifu ambao hakuna mahala kinapoeeleza muombaji namba moja Zitto .
Kiapo hiko hakina siani ya Zitto ambapo kina upungufu ambapo kimeambatanisha saini ya waombaji wawuli tu ambapo wametaka kwa udhaifu huo kesi hiyo iondelewe Mahakamani hapo.
“Muswada sio sheria mpaka usainewe ndio uweze kuwa sheria kwa sasa Bunge liachwe lifanye kazi yake kisheria na kwamba huo muswa haupo kwenye Ofisi ya Waziri mkuu wala Ofisi ya Mwanasheria Huu Muswada upo bungeni,” ameleeza.
Ameeleza kuwa wabunge wanauwezo wa kutoa maoni ya marekebisho bungeni kwa kuwawakilisha wananchi.
Upande wa watoa maomba uliongozwa na Wakili Mpare Mpoki umekitaka kifungu cha ibara ya 5 kwenye katiba inayoipa mahakama mamlaka ya kutengeu sheria au hatua yoyote itakayochukuliwa na Serikali au Mamlaka yoyote kwa kikiuka haki, uhuru na wajibu kama ilivyoanisha ibara ya 12 hadi 29 kwenye katiba.
Uamuzi wa Kesi hiyo utatolewa Jumatatu tarehe 14 Januari mwaka 2019.
Leave a comment