Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yawasilisha hoja 10, Mahakama kutoa maamuzi J’tatu
Habari za Siasa

Serikali yawasilisha hoja 10, Mahakama kutoa maamuzi J’tatu

Spread the love

SERIKALI imewasiliasha hoja 10 kesi ya kupinga Muswa wa Sheria ya vyama vya siasa iliyofunguliwa na Zitto Kabwe Kiongozi wa ACT-Wazalendo wa Wenzake. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Waombaji wengine ni Joran Bashange Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wanachi (CUF) Bara na Salim  Biman Mkuregenzi wa Mawasiliano ya Umma (CUF).

Moja ya hoja zilizowasilishwa na serikali kuwa Katiba ya Nchi imegawa mamlaka na kuyaheshimu.

Akiongoza jopo la Mawakili , Wakili Mkuu wa Serikali Mark Mulwambo mbele ya Jaji Benhajo Masoud ameeleza kuwa muhimuli wa Mahakama hauwezi kuingilia Muhimili wa Bunge katika kujadilia mambo yake.

Wakili ameleza kuwa amahakama inaweza kujadili sheria iliyotungwa na Bunge sio muswada ambao haujapitishwa kuwe sheria.

Hoja nyengine ya Serikali ni kwamba waombaji wamewasilisha maombi yao kwa kiapi chenye udhaifu ambao hakuna mahala kinapoeeleza muombaji namba moja Zitto .

Kiapo hiko hakina siani ya Zitto ambapo kina upungufu ambapo kimeambatanisha saini ya waombaji wawuli tu ambapo wametaka kwa udhaifu huo kesi hiyo iondelewe Mahakamani hapo.

“Muswada sio sheria mpaka usainewe ndio uweze kuwa sheria kwa sasa Bunge liachwe lifanye kazi yake kisheria na kwamba huo muswa haupo kwenye Ofisi ya Waziri mkuu wala Ofisi ya Mwanasheria Huu Muswada upo bungeni,” ameleeza.

Ameeleza kuwa wabunge wanauwezo wa kutoa maoni ya marekebisho bungeni kwa kuwawakilisha wananchi.

Upande wa watoa maomba uliongozwa na Wakili Mpare Mpoki umekitaka kifungu cha ibara ya 5 kwenye katiba inayoipa mahakama mamlaka ya kutengeu sheria au hatua yoyote itakayochukuliwa na Serikali au Mamlaka yoyote kwa kikiuka haki, uhuru na wajibu kama ilivyoanisha ibara ya 12 hadi 29  kwenye katiba.

Uamuzi  wa Kesi hiyo utatolewa Jumatatu tarehe 14 Januari mwaka 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

error: Content is protected !!