Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yatoa Bil 688 mradi wa umeme Rufiji
Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa Bil 688 mradi wa umeme Rufiji

Spread the love

SERIKALI imetoa kiasi cha Shilingi 688.6 bilioni, kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya Mto Rufiji. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dotto James, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango leo tarehe 24 Aprili 2019, amekabidhi hundi ya kiasi hicho cha fedha kwa mkandarasi anayejenga mradi huo, Kampuni ya Arab Contractors ya nchini Misri, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kukabidhi hundi hiyo James amesema, malipo hayo ni sehemu ya kwanza na kwamba yamegawanyika katika sehemu mbili.

“Malipo haya ya awali yataenda sambamba na malipo mengine ambapo jumla take itakuwa shillingi tilioni 1 kwa ujumla” amesema James.

Naye  Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas kupitia taarifa yake aliyoitoa katika ukurasa wake wa Twitter, amesema lengo la serikali la kutoa fedha hizo ni kuhakikisha kwamba hali ya upatikanaji wa nishati ya umeme inaimarika kwa ajili ya kusaidia kukuza kasi ya uchumi wa viwanda kwa ajili ya kubadili maisha ya Watanzania.

“Serikali yatoa mabilioni kuanza utekelezaji wa mradi wa Umeme wa Maji Rufiji, lengo ni kuihakikishia nchi umeme wa kutosha, kusaidia kasi ya uchumi wa viwanda na kuyabadili maisha ya Mtanzania mmoja mmoja,” inaeleza taarifa hiyo ya  Dk. Abbas.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Polisi waendelea kuwabana wanavunja sheria, operesheni 3D yaendelea

Spread the love  JESHI la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Kimeendelea na...

Habari Mchanganyiko

Jela miaka 25 kwa kukutwa na kilo 107.29 za bangi

Spread the love  MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, kanda ya Morogoro imemhukumu miaka...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yamhukumu mwandishi wa habari kifungo cha miezi 6

Spread the loveMahakama ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imemhukumu kifungo cha...

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

error: Content is protected !!