Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali yaomba wadau kukarabati nyumba za walimu
Elimu

Serikali yaomba wadau kukarabati nyumba za walimu

Mwita Waitara
Spread the love

NAIBU Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mwita Waitara ametoa wito kwa wananchi na wadau wa maendeleo kushirikiana na serikali katika kukarabati nyumba za walimu nchini. Anaripoti Danson Kaijage … (endelea).

Waitara ametoa wito huo leo tarehe 12 Aprili 2019 bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje aliyehoji  mpango  wa serikali katika kuboresha nyumba za walimu pamoja na shule kongwe katika jimbo lake.

Akijibu swali hilo, Waitara amesema nyumba za walimu zinazohitaji kufanyiwa ukarabati ni nyingi na kwamba uwezo wa serikali si mkubwa, na kuwaomba wadau kutoa michango yao katika kufanikisha ukarabati wa nyumba za walimu nchini.

Hata hivyo, Waitara  amesema katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2019/2020 wizara yake imetenga kiasi cha fedha , kwa ajili ya ukarabati wa nyumba za walimu na shule kongwe nchini.

“Si kweli kwamba tunakarabati shule tu,  isipokuwa ukweli ni kwamba tunakarabati  shule nyingi kuliko nyumba za walimu, hata kwenye kitabu cha bajeti ya mwaka huu tunachojadili sasa  yako maeneo ya kupitia katika majimbo mbalimbali,” amesema na kuongeza Waitara.

“Tumetaja  maeneo hayo na fedha zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa nyumba za walimu. Uwezo wa serikali si mkubwa sana tunaomba mheshimiwa mbunge na wadau mbalimbali tushirikiane katika jambo hilo ili kupunguza shida ya walimu.”

Aidha, Waiatara amesema serikali itaendelea kukarabati miundombinu ya elimu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!