Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yamwaga ajira sekta ya Afya
Afya

Serikali yamwaga ajira sekta ya Afya

Waziri wa Muungano, Suleiman Jafo
Spread the love

SERIKALI imetoa ajira mpya za watumishi kada za afya katika Mamlaka za serikali za Mitaa  (TAMISEMI) 6180 kwa mwaka wa fedha 2018/19. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma,  Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa, Suleiman Jafo amesema ajira hizo ni utekelezaji wa  ahadi ya serikali katika kuboresha huduma ya afya.

Jafo amesema kuwa ajira zao zimetokana na kibali kilichoandikwa kwa serikali cha kuajili watumishi wa kada mbalibali wa sekta ya afya nchini.

“Kibali hiki ni mwendelezo wa kibali cha ajira kwa kada za afya 3152 kilichotolewa mwezi Julai 2017 kwa lengo la kukabiliana na changamoto za utumishi katika vituo vya afya nchini.

“Napenda kiwataarifu kuwa serikali imekamilisha mchakato wa ajira ya watumishi 61,800 wa kada mbalibali za afya ikiwemo madaktari, wafamasia, wataalamu wa maabara, wauguzi, utabibu wa huduma wa afya na wataalamu wengine wa sekta ya afya ambapo watumishi hao wamepangwa katika Manlaka za serikali za Mitaa zote ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za afya nchini,” amesema Jafo.

Aidha amesema zipo baadhi ya kada zilizokosa waombaji wenye sifa kuwa ni,wahandisi wa vifaa tiba, maofisa wauguzi ngazi ya shahada, wataalamu wa mionzi, madaktari wa meno na wataalamu wa viungo bandia.

“Nawashauri wananchi kusomea taaluma hizo kwani mahitaji ni makubwa mno katika vituo vya kutolea huduma nchi,” amesema Jafo.

Jafo amesema kuwa mgawanyo  wa watumishi umezingatia halmashauri zenye hospitali,vituo vya afya na zahanati zilizokamilika lakini zilikuwa hazifanyi kazi ipasavyo kwa kukosa watumishi.

Amesema kuwa mgawanyo umezingatia vituo vya afya 210 vilivyoboreshwa katika halmashauri mbalimbali ili kuziwezesha kutoa huduma zilizokusudiwa.

Hata hivyo Jafo ametoa wiki mbili kwa watumishi waliochaguliwa kuwa wameisha fika katika vituo vyao vya kazi na kama kuna mtu ambaye atafika katika kituo chake cha kazi ndani ya siku 14 nafasi yake atapewa mtu mwingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!