SERIKALI imekiri kuwepo kwa udhaifu katika uchukuaji fomu, kwa ajili ya kugombea nafsi mbalimbali kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari Jumatano tarehe 30 Oktoba 2019, Seleman Jafo, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) amesema, siku ya kwanza katika uchukuaji fomu imekumbana upungufu kadhaa.
Kauli hiyo inakuja huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kikiwa tayari kimemwandikia Jafo na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kulalamikia hujuma zinazofanywa na waliopewa mamlaka ya kusimamia zoezi hilo.
Waziri huyo, amewataka waliopewa mamlaka kuhakikisha wanakabiliana na malalamiko hayo na kwamba, tayari ofisi yake imepokea malalamiko zaidi ya 70 kwa siku hiyo ya kwanza na inashughulikia malalamiko hayo.
Mapema jana, Chadema kililalamikia mazingira mabovu, vitimbi na hujuma zinazofanywa kwa wagombea wake wakati na baada ya kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi huo.
“Kufuatia matukio yanayoonesha mazingira ya kuharibu uchaguzi wa serikali za mitaa yaliyojitokeza siku ya kwanza ya kuchukua, kujaza na kurejesha fomu za uteuzi kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo, siku ya Jumanne Oktoba 29, 2019,” aimeeleza na kuongeza;
“Chadema kimemwandikia barua Waziri Jafo, kumtaka achukue hatua za haraka dhidi ya ukiukwaji mkubwa wa taratibu zinazosimamia uchaguzi huo,” alieleza Tumaini Makene, Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya chama hicho.
Miongoni mwa malalamiko ya Chadema ni wasimamizi na wasaidizi wa uchaguzi kutoa nakala za fomu zisizokuwa na nembo ya halmashauri na mhuri husika, ili kuthibitisha kuwa ni nakala halisi, kutofunguliwa kwa ofisi kwa ajili ya kutoa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea.
Leave a comment