Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaizuia mitambo ya kampuni ya madini
Habari Mchanganyiko

Serikali yaizuia mitambo ya kampuni ya madini

Waziri wa Madini, Dotto Biteko
Spread the love

SERIKALI imeiagiza Tume ya Madini Tanzania, kuzuia mali na mitambo yote ya Kampuni ya Canaco inayomiliki leseni ya Uchimbaji Madini ya dhahabu, kutokana na kukiuka masharti ya leseni hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Pia, Waziri Biteko ameagiza kampuni hiyo iliyoko katika Kijiji cha Magambazi Wilayani Handeni Mkoani Tanga, ipewe hati ya makosa kwa sababu ya kwenda kinyume na Sheria ya Madini yam waka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 pamoja na kanuni za mwaka 2018.

Sambamba na hilo, aliumuelekeza Kamishna wa Tume ya Madini Dkt.Athanas Macheyeka kumpa mwekezaji huyo hati ya makosa (default notice) kwa ajili ya kurekebisha makosa waliyonayo kwenye leseni ya uchimbaji wa madini na kama watashindwa kurekebisha makosa kwa muda uliotajwa na sheria, leseni yao ifutwe wapewe wawekezaji wengine.

Katika hatua nyingine, Waziri Biteko aliagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi katika sakata la utoroshwaji wa Carbon zenye madini ambazo ziliibwa usiku kutoka eneo hilo na kupelekwa mkoani Mwanza kwa ajili ya kuyeyushwa ili kupata dhahabu kinyume cha utaratibu.

Waziri Biteko alisema kuwa mwekezaji huyo awali alifika katika Wizara ya Madini na kuomba kibali cha kusafirisha carbon tani 2.23 kwenda mkoani Mwanza katika kiwanda cha JEMA AFRICA LTD kwa ajili ya kuchenjuliwa lakini wakanyimwa kutokana na matatizo yao ya ndani lakini baadae wakachukua kibali cha kughushi kutoka Dodoma kwa ajili ya kusafirishia carbon kupeleka Mwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!