Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yagoma kuwalipa fidia waliokutwa vyeti feki kimakosa
Habari za Siasa

Serikali yagoma kuwalipa fidia waliokutwa vyeti feki kimakosa

Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda
Spread the love

SERIKALI  imesema hakuna mfanyakazi aliyeondolewa kazini kimakosa katika zoezi la uhakiki wa vyeti feki, zaidi ya kurudishwa kazini. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Joseph Kakunda alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Ziwani, Nassor Suleiman Omari (CUF), aliyehoji serikali imewarejesha walimu wangapi  kazini ambao wameathirika na kukumbwa na kukutwa na vyeti feki  kimakosa.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri, Kakunda amesema kuwa ni kweli kulikuwepo na manung’uniko kwa baadhi ya watumishi wa sekta ya walimu ambao walikutwa katika mkumbo wa feti kimakosa.

Amesema kuwa walimu hao walikata rufaa na walimu wapatao 1907 walioonekana kuwa waliingizwa kimakosa katika mfumo wa vyeti feki walirudishwa kazini.

Aidha amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 na mwaka 2017/18 serikali ilifanya uhakikia wa vyeti vya watumishi wa Umma ili kubaini waliokuwa na vyeti halali na waliokuwa na vyeti vya kugushi.

Amesema katika uhakiki huo, jumla ya walimu 3,655 walibainika kuwa na vyeti vya kugushi na walipoteza sifa za kuendelea kuwa watumishi wa Umma.

Mbali na hilo amesema wale wote ambao walibainika kuwa na vyeti feki hata kama walikuwa wanakaribia kustaafu hawatalipwa mafao yoyote kwani serikali imewasemehe kuwashikati kwani watu hao walitakiwa kushitakiwa kwa kosa la jinai.

Naibu Waziri, Kakunda amesema katika harakati za kuziba pengo la walimu waliondolewa kazini, ndani ya miaka miwili serikali imeajiri jumla ya walimu 6495.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!