Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine aachiwa huru, akamatwa tena
KimataifaTangulizi

Bobi Wine aachiwa huru, akamatwa tena

Bobi Wine
Spread the love

SERIKALI ya Uganda imemuondolea mashtaka Mbunge wa Kyadondo, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, lakini alikamatwa tena muda mfupi baada ya kuachiwa huru. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Bob Wine leo Alhamisi tarehe 23 Agosti, 2018 alitarajiwa kurudishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu Kaskazini mwa Uganda.

Uamuzi huo unadhaniwa kushinikizwa na hatua ya jumuiya za kimataifa zilizoishinikiza serikali ya Uganda kumuachia huru Bob Wine.

Kabla ya Serikali ya Uganda kutangaza kumuondolea mashitaka Bob Wine, mawakili wake walijuzwa kuwa kesi ya mwanasiasa huyo machachari itasikilizwa katika kambi ya Kijeshi ya Makindye alikokuwa anazuiliwa Bob Wine.

Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na inaarifiwa kwamba anatarajiwa kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa.

Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo aliwasilishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.

Mawakili wake awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala. Kumekuwa na shinikizo kubwa kimataifa la kutaka Bobi Wine aachiwe huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!