Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali ya Tanzania yatoa maelekezo ulipaji ada shule binafsi
ElimuTangulizi

Serikali ya Tanzania yatoa maelekezo ulipaji ada shule binafsi

Prof. Joyce Ndalichako
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema, ada za shule nchini humo zilipwe kulingana na makubaliano yaliyofikiwa mwanzoni mwa mwaka wa masomo 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaaam … (endelea).

Kauli hiyo ya Serikali, imetolewa leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020 na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikielezea maelekezo ya ulipaji ada za shule binafsi baada ya janga la corona.

Maelekezo hayo yanatolewa kipindi ambacho kumekuwa na mivutano kwa baadhi ya shule binafsi na wazazi au walezi juu ya gharama wanazopaswa kulipwa pindi shule zitakapofunguliwa Jumatatu ya tarehe 29 Juni 2020.

Shule zote za msingi na sekondari zinafunguliwa baada ya kufungwa kuanzia tarehe 17 Machi 2020 ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19).

“Wizara inaelekeza na kusisitiza, wanafunzi wote wapokelewe kwa ajili ya kuendelea na masomo ifikapo tarehe 29 Juni 2020,” inaeleza taarifa hiyo ya wizara iliyotolewa na Sylvia Lupembe, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara hiyo.

Sylvia amesema, kulinga na ratiba iliyotolewa na wizara, wanafunzi wanatarajiwa kukamilisha masomo kama inavyoelekezwa na mihtasari ya madarasa waliyopo.

“Hivyo, ada za shule zilipwe kulingana na makubaliano yaliyofikiwa mwanzoni mwa mwaka wa masomo. Wizara inaendelea kusisitiza maelekezo ya awali kwamba kusiwepo na nyongeza yoyote katika kiwango cha ada,” amesema

Katika taarifa hiyo, inasema “wazazi pia wanatakiwa kuzingatia kiwango cha ada huwa kinakadiriwa kwa kuzingatia gharama mbalimbali za uendeshaji wa shule, gharama ambazo ziliendelea kuwepo hata muda ambao shule zilikuwa zimefungwa.”

“Gharama hizi ni pamoja na mishahara ya watumishi, Ankara za umeme na maji,” amesema Sylvia.

Kuhusu malipo ya chakula na usafiri, “wizara inazielekeza kamati/bodi za shule kufanya uchambuzi wa gharama inayopaswa kupungua kwa siku ambazo wanafunzi hawakuwa shuleni. Tathimini hii izingatie ratiba mpya ya mihula iliyotolewa na wizara.”

Taarifa hiyo imesema, kulingana na Sheria ya Elimu, Sura Na. 353 (RE 2002), uendeshaji wa shule unasimamiwa na kamati/bodi za shule, vyombo ambavyo vimeundwa kwa mujibu wa sharia hiyo.

“Hivyo, wamiliki wa shule wanaelekezwa kuzingatia sharia hiyo na kuzipa nafasi bodi/kamati za shule kutekeleza majukumu kulingana na sharia iliyoziunda.”

“Kwa kuzingatia kwamba, Serikali ilifunga shule wakati muhula wa masomo ukiwa unaendelea, wizara inaelekeza kwamba wanafunzi wote wapokelewe na kuendelea na masomo yao bila kikwazo chochote ili kukamilisha muhula huo,” imeeleza

1 Comment

  • Tahadhari kuhusu virusi vya Corona

    Ni kunawa mikono tu? Au pia na kuvaa barakoa na kutokukaribiana? Wataalamu wa afya wanasemaje?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!