Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Mgonjwa wa kwanza wa Corona agundulika Tanzania
AfyaHabari Mchanganyiko

Mgonjwa wa kwanza wa Corona agundulika Tanzania

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeripoti kuwepo mgonjwa mmoja mwenye ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na Virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uwepo wa mgonjwa huyo imetolewa leo tarehe 16 Machi 2020, Waziri Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, wakati akizungumza na wanahabari.

Waziri Ummy amesema mgonjwa huyo ambaye ni raia wa Tanzania, aliingia nchini tarehe 15 Machi 2020, akitokea nchini Ubelgiji kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) .

Amesema mgonjwa huyo mnamo tarehe 3 Machi mwaka huu aliondoka nchini na kwenda katika nchi za Sweden na Denmark alikokuwa kati ya tarege 5 hadi 13 Machi 2020.

“Alipowasili akafanyiwa ukaguzi na kuonekana kutokuwa na homa baadae alianza kujisikia vibaya akiwa hotelini na kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru ambapo sampuli ilipelekwa maabara ya taifa ya afya ya jamii iliyopo Dar es Salaa kwa ajili ya uchunguzi,” amesema Waziri Ummy na kuongeza:

“Vipimo vya maabara vimethibitisha kuwa mtu huyu ana maambukizi ya ugonjwa wa Corona. Mgonjwa anaendelea vizuri na matibabu.”

Waziri Ummy amewataka Watanzania kuchukua hatua juu ya janga hilo kwa kufuata ushauri unaotolewa na mamlaka za afya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!